SILAA AZURU KILIMANJARO KUKAGUA MAWASILIANO, MKOMAZI YAPEWA KIPAUMBELE

 


 ðŸ“ŒNa Mwandishi Wetu,

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jerry William Silaa amewasili katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro kwa ziara ya kikazi ya siku moja, ambapo amepokelewa rasmi na mwenyeji wake, Nurdin Babu, Mkuu wa Mkoa huo.

Lengo kuu la ziara ya Waziri Silaa ni kukagua na kutathmini hali ya upatikanaji wa huduma za mawasiliano katika Mkoa wa Kilimanjaro, hususan katika eneo la Mkomazi.

Akizungumza mara baada ya kuwasili,  Silaa amesisitiza umuhimu wa kuhakikisha kila Mtanzania, popote alipo, anapata huduma bora na ya uhakika ya mawasiliano, akieleza kuwa mawasiliano ni msingi wa maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Kwa upande Nurdin Babu, Mkuu wa Mkoa huo amemkaribisha Waziri Silaa kwa niaba ya wananchi wa Kilimanjaro na kupongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kupitia Wizara hiyo katika kuboresha miundombinu ya mawasiliano nchini kote.

Katika ziara hiyo, Waziri Silaa anatarajiwa kutembelea maeneo mbalimbali ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro ili kujionea changamoto zilizopo, mafanikio yaliyopatikana, pamoja na kufanya mazungumzo na wananchi kwa lengo la kupata mrejesho wa moja kwa moja kuhusu huduma za mawasiliano.




Post a Comment

0 Comments