MCHENGERWA: HAKUNA SABABU MIRADI KUKWAMA, FEDHA ZIPO

 



 ðŸ“ŒBAHATI MSANJILA


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa, amewataka wakandarasi wazawa kuhakikisha miradi ya miundombinu ya barabara vijijini na mijini inatekelezwa kwa ubora na ufanisi. 

 

Ameyasema hayo jijini Dodoma, wakati akizindua mafunzo ya uwezeshaji kwa wakandarasi wanaotekeleza miradi ya TARURA kupitia Mfumo wa Samia Infrastructure Bond.

 

Mchengerwa amesema kuwa fedha kupitia bond hiyo zinatosha kutekeleza miradi yote, hivyo hakuna sababu ya miradi kushindwa kukamilika. 

 

Aidha, amebainisha kuwa Samia Infrastructure Bond ni suluhisho la changamoto ya mitaji kwa wakandarasi wazawa huku akiitaka TARURA kuanza kuwalipa wakandarasi 322 waliobaki kuanzia Aprili 11, 2025, baada ya serikali kuwalipa wakandarasi 457, ili kuwe na usawa na haki kwa wote.

 

Kaimu Mtendaji Mkuu wa TARURA, Edward Kambona, amesema taasisi hiyo itaendelea kushirikiana na CRDB na wakandarasi wazawa kukamilisha miradi kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa.

Post a Comment

0 Comments