BUNGE KUKUSANYA BIL. 3 KWA AJILI YA SHULE YA WAVULANA DODOMA


 ðŸ“ŒBAHATI MSANJILA


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametangaza kuwa kupitia Bunge Marathon 2025, Bunge linatarajia kukusanya Sh bilioni 3 kwa ajili ya ujenzi wa shule ya wavulana ya Bunge itakayojengwa Kikombo, Dodoma.

Akizungumza kwenye uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma, Majaliwa amesema shule hiyo itakuwa ya kisasa yenye miundombinu yote kama madarasa, mabweni, maabara, nyumba za walimu na viwanja vya michezo.

Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson amesema hii ni marathon pekee inayojumuisha Wabunge wote wa majimbo 264, na inalenga kuleta mabadiliko ya kweli kwenye elimu ya mtoto wa kiume.

Dkt. Tulia Ackson amewashukuru wadau mbalimbali kwa mchango wao katika kufanikisha mpango wa ujenzi wa shule ya wavulana ya Bunge kwa ngazi ya kidato cha tano na sita.

Mwenyekiti wa Bunge Marathon 2025, Festo Sanga ambaye pia ni Mbunge wa Makete, Sanga ameeleza kuwa mbio hizo za hisani ni zao la maono ya Spika Tulia Ackson, zikiwa na lengo la kuendeleza jitihada za maendeleo ya elimu kwa watoto wa kiume baada ya kukamilisha shule ya wasichana.

Zaidi ya wakimbiaji 5,000 wamejitokeza kushiriki mbio hizo za hisani, zikiwa ni mwendelezo baada ya ujenzi wa shule ya wasichana ya Bunge.






Post a Comment

0 Comments