📌Na Mwandishi Wetu,
Wataalamu wa kudhibiti ujangili wa Wanyamapori na mazao ya misitu kutoka nchi
za Malawi, Zambia na Tanzania wamekutana Jijini Dar Es Salaam kwa lengo la
kujengewa uwezo na kubadilishana uzoefu wa kudhibiti ujangili wa wanyama pori
na mazao ya misitu ndani ya nchi na kwenye maeneo ya mipakani.
Akifungua mafunzo hayo Naibu Waziri wa Maliasil na Utalii, Dunstan
Kitandula(Mb) amesema kuwa ushirikiano katika kudhibiti ujangili wa wanyamapori
na mazao ya misitu ni jambo la msingi kwa nchi wanachama wa mkataba wa
Lusaka.
Amesisitiza kuwa unganishaji nguvu ya
pamoja katika mapambano dhidi ya changamoto ya ujangiri wa wanyamapori ndani ya
nchi wanachama na sehemu za mipakani haunabudi kuimarishwa hasa ikizingatiwa
kuwa nchi za Tanzania, Zambia na Malawi zinaunganishwa na mifumo ikolojia ya
Kasungu - Luambe na Luangwa kusini katika mpaka wa Malawi na Zambia; na
halikadhalika mfumo ikolojia wa miombo ambao unapatikana kusini mwa Tanzania na
mashariki ya Zambia na Malawi.
Kitandula ameongeza kuwa ili kulinda Rasilimali hizi uimarishaji wa sheria na
kanuni zinazosimamia uhifadhi wa wanyamapori na misitu katika Nchi wananchama
wa Mkataba wa Lusaka haunabudi kutiliwa mkazo. Katika eneo hili, amesema nchi
ya Tanzania imejipambanua kuwa kinara kwa kuzifanyia mabadiliko sheria zake ili
kuziongezea makali ziweze kutoa adhabu kali kwa watu wanaotiwa hatiani kwa
kufanya makosa ya ujangili na biashara haramu ya usafirishaji wa wanyamapori na
mazao ya misitu.
Akimkaribisha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mkurugenzi wa Kikosi Kazi
cha Mkataba wa Lusaka Ndugu Edward Phiri amesema serikali ya Tanzania kwa
kuruhusu mafunzo hayo kufanyikia nchini Tanzania.
0 Comments