UVCCM YAHIMIZA UCHAGUZI WA VIONGOZI WENYE UTU SI UCHU WA MADARAKA



📌BAHATI MSANJILA


Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) umeahidi kuhakikisha jumuiya hiyo inachochea ushindi wa kishindo kwa CCM kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu kwa kuandaa midahalo mbalimbali ili kueleza mafanikio yaliyopatikana chini ya Serikali ya Awamu ya Sita.

 

Ili kufanikisha hilo, UVCCM imewataka vijana kushiriki kikamilifu na kuhamasisha wenzao kushiriki maboresho ya Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ili wapate haki ya kupiga kura kwenye uchaguzi ujao.

 

Katibu wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi wa UVCCM Taifa, Jessica Mshama, ametoa ahadi hiyo jijini Dodoma baada ya kupokelewa rasmi katika Makao Makuu ya jumuiya hiyo. Amesema vijana wanapaswa kuwa mabalozi wa Taifa kwa kuchagua viongozi wenye utu badala ya wale wenye uchu wa madaraka.

 

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Utawala na Uendeshaji wa UVCCM Makao Makuu, Amina Kaumo, na Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Dodoma, Abdulhabib Mwanyemba, wameahidi kushirikiana kikamilifu kuhakikisha kura za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan zinapatikana kwa wingi.

 

Katibu huyo aliteuliwa na Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kushika nafasi hiyo Februari 21 mwaka huu, na sasa anajipanga kuimarisha uhamasishaji wa vijana kuelekea uchaguzi.










Post a Comment

0 Comments