UCSAF YATEKELEZA MAONO YA RAIS SAMIA, MINARA 758 KUJENGWA MEI




  📌BAHATI MSANJILA

Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) umeendelea kuimarisha miundombinu ya kidigitali nchini, ambapo hadi sasa vijiji 1,407 katika kata 713 kwenye wilaya 127 za mikoa 26 ya Tanzania Bara vimenufaika na mradi huo, huku wananchi milioni 8.5 wakitarajiwa kufikiwa na huduma hizo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Afisa Mtendaji Mkuu wa UCSAF, Mhandisi Peter Mwasalyanda, amesema utekelezaji wa mradi huu umewezeshwa na ruzuku ya shilingi bilioni 126 iliyotolewa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ili kusaidia watoa huduma za mawasiliano kueneza mtandao vijijini.

Kwa mujibu wa Mwasalyanda, hadi kufikia Mei 2025, jumla ya minara 758 itakuwa imejengwa, ambapo minara 430 tayari inatoa huduma kwa wananchi. Aidha, ruzuku ya shilingi bilioni 5.5 imetolewa ili kuongeza nguvu katika ujenzi wa minara mingine 304.

Katika jitihada za kukuza ushiriki wa mabinti kwenye masomo ya sayansi na TEHAMA, UCSAF imeanzisha programu maalum ya Msichana na TEHAMA. 

Mpaka sasa, walimu 1,585 wamepewa mafunzo maalum, huku wasichana 1,204 wakishiriki mafunzo mbalimbali ya TEHAMA ili kuwajengea uwezo wa kushiriki kikamilifu katika sekta ya teknolojia.

Kwa upande mwingine, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, amesema kuwa hadi kufikia Machi 27, 2025, taasisi 35 tayari zimewasilisha taarifa za mafanikio yao kwa kipindi cha miaka minne. 

Mafanikio haya yanatokana na maono na dhamira ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, hususan kupitia slogan yake ya 4R.

Aidha, Msigwa Ameeleza kuwa kuanzia Aprili 14, 2025, mawaziri wa wizara mbalimbali wataanza kuwasilisha mafanikio ya sekta zao kwa umma.

Post a Comment

0 Comments