UCSAF YABORESHA MAWASILIANO KANDA YA KATI KWA KUSIMIKA MINARA 148


 


        📌BAHATI MSANJILA


Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) umeendelea kuboresha huduma za mawasiliano nchini kwa kusimika jumla ya minara 148 katika Kanda ya Kati, ambapo 78 kati yake tayari imewashwa na inafanya kazi.

 

Kwa mujibu wa taarifa kutoka  UCSAF, mikoa iliyofaidika na mpango huu ni Dodoma Minara 36 na 25 imewashwa, Singida 32 minara, 14 imewashwa, Iringa 22 minara, 10 imewashwa, Tabora 50 minara, 23 imewashwa, na Kigoma 8 minara, 6 imewashwa.

 

Mpango huu ni sehemu ya jitihada za Serikali kuhakikisha wananchi wote, hususan walioko vijijini, wanapata huduma bora za mawasiliano, hivyo kuwezesha maendeleo ya kijamii na kiuchumi kupitia teknolojia ya mawasiliano.


Post a Comment

0 Comments