📌Na Mwandishi Wetu
Akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dodoma Waziri
wa Afya Jenista Mhagama amesema Tanzania inakwenda kwenye uchaguzi huu ikiwa na
matumaini makubwa ya ushindi, ikiegemea diplomasia imara na sifa za Prof.
Janabi katika kuleta mageuzi kwenye sekta ya afya.
Prof. Janabi, ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya
Taifa Muhimbili (MNH) na Mshauri wa Rais wa Masuala ya Afya na Lishe, ana
uzoefu mkubwa katika sekta ya afya, ikiwa ni pamoja na kuanzisha na kuiongoza
Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI).
Katika uchaguzi huu, Prof. Janabi atachuana na wagombea kutoka
Togo, Ivory Coast, na Guinea Conakry.
Katika hatua nyingjne Jenista ametoa wito kwa Watanzania na
wadau wa afya kumuunga mkono mgombea wa Tanzania kwa kampeni za kidiplomasia na
dua.
Tanzania ilishinda nafasi ya Mkurugenzi wa WHO Kanda ya Afrika
Agosti 2024 kupitia Marehemu Dkt. Faustine Ndugulile, lakini kabla ya kuanza
majukumu yake, alifariki dunia Novemba 27, 2024. Kufuatia pengo hilo, Tanzania
imemteua Prof. Mohamed Janabi kuwania nafasi hiyo ili kuendeleza mchango wa
nchi katika kuboresha afya barani Afrika.
Serikali ya Tanzania, kwa kutambua umuhimu wa nafasi hii,
imefanya maamuzi ya haraka kwa kumteua Prof. Mohamed Janabi, mtaalamu
mashuhuri wa afya na kiongozi mwenye uzoefu mkubwa, kuendelea na harakati za
kuwania nafasi hiyo ili kuhakikisha Tanzania inaendelea kushikilia nafasi yake
ndani ya WHO.
Prof. Janabi alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa kwanza wa
Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), ambapo alifanya mageuzi makubwa
yaliyosaidia kupunguza rufaa za wagonjwa wa moyo kwenda nje ya nchi kwa zaidi
ya asilimia 95.
Aidha, kama Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa
Muhimbili (MNH) na Mshauri wa Rais wa Masuala ya Afya na Lishe,
amechangia kwa kiasi kikubwa katika uboreshaji wa huduma za afya nchini
Tanzania na Barani Afrika kwa ujumla.
Prof. Janabi pia amehusika katika tafiti mbalimbali za afya za
kitaifa na kimataifa, amekuwa mhadhiri wa tiba katika Chuo Kikuu cha Muhimbili (MUHAS)
na mshauri wa masuala ya afya katika mashirika ya kimataifa.
Katika uchaguzi huu, Prof. Janabi atachuana na wagombea kutoka
Togo, Ivory Coast, na Guinea Conakry.
Tanzania sasa inaelekeza nguvu zake katika kampeni za mwisho
kuelekea uchaguzi wa Mei 18, 2025, huku ikiendelea kushirikiana na mataifa
mengine ili kuhakikisha ushindi wa Prof. Janabi.
0 Comments