RAIS SAMIA AWEKEZA BILIONI 126 KUBORESHA MAWASILIANO VIJIJINI, MINARA 758 KUWASHWA MEI 2025

 



 

📌BAHATI MSANJILA


Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jerry Silaa, ameagiza kukamilika kwa ujenzi wa minara 758 ya mawasiliano vijijini ifikapo Mei 12, 2025, na kuhakikisha yote imewashwa ili wananchi waanze kunufaika na huduma za mawasiliano.

 

Akizungumza katika ziara ya ukaguzi wa mradi huo katika Kijiji cha Kidete, Wilaya ya Kilosa, Morogoro, Waziri Silaa amesema kuwa Serikali imetenga Shilingi bilioni 126 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo, ambao utapunguza changamoto ya mawasiliano nchini.

 

Amesisitiza kuwa mradi huu ni sehemu ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Uchumi wa Kidijitali (2024-2034) uliozinduliwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ukiwa na lengo la kuboresha miundombinu ya mawasiliano.

 

Hadi sasa, minara 420 kati ya 758 imekamilika, ikiwa ni zaidi ya asilimia 55 ya utekelezaji wa mradi huo, ambao unatarajiwa kunufaisha wananchi milioni 8.5 waishio vijijini.







Post a Comment

0 Comments