NAIBU WAZIRI MAHUNDI APONGEZA HUDUMA ZA MAWASILIANO KATIKA MPAKA WA TUNDUMA

 




       ðŸ“ŒNa Mwandishi wetu

Naibu Waziri wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Maryprisca Mahundi  amepongeza uwepo kwa huduma bora za mawasiliano ya simu na intaneti katika eneo la forodha lililopo katika mpaka wa Tunduma.


Naibu Waziri Mahundi ametoa pongezi hizo wakati wa ziara yake ya kukagua upatikanaji wa huduma za mawasiliano maeneo ya mipakani leo, Machi 21, 2025, katika mpaka wa Tunduma mkoani Songwe.

Mhe. Mahundi ametumia fursa hiyo kuisisitiza kampuni ya Airtel Tanzania kukamilisha ujenzi wa mnara wa mawasiliano ya simu kupitia Mradi wa Tanzania Kidijitali katika Wilaya ya Momba, hasa katika Kata ya Nzoka, Kijiji cha Namtambala, ili kuboresha huduma za Mawasiliano katika eneo husika.

Akitoa salamu, Mkuu wa Wilaya ya Momba, Elias Mwandobo, ameipongeza wizara kwa juhudi zake katika kuboresha huduma za mawasiliano, pamoja na kutoa rai kwa wananchi kutumia huduma hizi ili kujipatia maendeleo, ikiwemo sekta ya kilimo.

Naye, Bw. Nsajigwa Mwambegele, Meneja Msaidizi wa Idara ya Forodha Mkoa wa Songwe, ameishukuru serikali kupitia Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kwa kuwezesha huduma bora katika eneo hilo.





Post a Comment

0 Comments