DKT. JINGU AKUTANA NA SOS CHILDREN'S VILLAGE

 





   ðŸ“ŒNa Mwandishi Wetu,

Katibu Mkuu wa Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wanawake na Makundi Maalum Dkt. John Jingu amepokea ugeni kutoka Shirika la Watoto la SOS Children's Village ambapo ugeni huo ukiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo Aisha Salim Ali katika Ofisi za Wizara jijini Dodoma.

Dkt Jingu amelipongeza Shirika hilo kwa jitihada zake za kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha wanadhibiti changamoto ya watoto kuishi na kufanya kazi mitaani baada ya Shirika hilo kukabidhi Mwongozo wa Taifa wa Uanzishaji, Uendeshaji na Usimamizi wa makao ya watoto nchini.

Aidha Dkt. Jingu ametoa wito kwa jamii kuimarisha taasisi ya familia na kuepuka migogoro kwani tafiti zinaonesha hivi karibuni kumekua na kuvunjika kwa ndoa nyingi na kupelekea kupatikana kwa wimbi la watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la SOS Children's Village Aisha Salim Ali ameahidi ushirikiano kati ya Shirika lake na Wizara katika kuhudumia Watoto katika Makao ya Watoto kwa kuweka namna nzuri ya Utoaji wa huduma na Malezi katika Makao hayo.






Post a Comment

0 Comments