📌BAHATI MSANJILA
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dkt. Amos Nungu, amesema serikali imewekeza Shilingi bilioni 25.7 katika utafiti, ubunifu, na maendeleo ya teknolojia katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita, hatua inayolenga kuimarisha sekta ya sayansi na teknolojia nchini.
Akizungumza jijini
Dodoma, Dkt. Nungu amesema kupitia uwekezaji huo, COSTECH imefadhili zaidi ya
tafiti 50 katika sekta za elimu, kilimo, afya, na mazingira, huku vituo vya
ubunifu 111 vikiimarishwa ili kuleta suluhisho la kisayansi kwa jamii.
Dkt Nungu amesema
Matokeo ya uwekezaji huu ni usajili wa kampuni mpya 70 zinazotokana na wabunifu
waliowezeshwa na serikali.
Aidha, serikali
imetenga Shilingi bilioni 6.3 kwa ajili ya miradi ya kukabiliana na mabadiliko
ya tabianchi na Shilingi milioni 600 kwa miradi minne ya usalama wa chakula,
ikiwemo udhibiti wa magonjwa ya mazao na uboreshaji wa uhifadhi wa
chakula.
Pia, kupitia Samia
Commercialization Fund, Shilingi bilioni 2.3 zimetolewa kusaidia wabunifu wa
Kitanzania kuingiza bunifu zao sokoni, hatua inayosaidia kuondoa changamoto ya
mitaji kwa wabunifu.
Katika kuhakikisha
Tanzania inabaki kwenye ushindani wa kimataifa, COSTECH imeanzisha kongano nane
bunifu katika mikoa mbalimbali, ikiwa ni sehemu ya mpango wa kuboresha sekta ya
viwanda na kilimo kwa kutumia teknolojia.
0 Comments