WANAWAKE HAKIKISHENI MALEZI BORA NA KULINDA MAADILI

 



📌BAHATI MSANJILA

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bara Steven Wasira, amewataka wanawake nchini kuhakikisha wanazingatia maadili bora na malezi mema kwa watoto wao, huku akisisitiza kuepuka maadili mabovu, ikiwa ni pamoja na kuhusisha mapenzi ya jinsia moja.


Wasira ameyasema hayo jijini dodoma wakati akizungumza kwenye kongamano kuelekea maadhimisho ya miaka 48 ya Chama cha Mapinduzi CCM lililoandaliwa na Umoja wa wanawake Tanzania (UWT).

Wasira amekumbusha maneno ya Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda aliyosema kuhusu mapenzi ya jinsia moja, akisema kuwa iwapo atakutana na wanaume wanaoshirikiana kimapenzi, atawafunga jela na kuwaondoa kama wanaume, akielezea kuwa hali hiyo ni kinyume na maumbile na haiwezi kukubalika.

Katika hotuba yake, Wasira amewataka wanawake kuwa macho na kuhakikisha wanalea watoto kwa misingi bora ili kuwaepusha na ushawishi wa maadili mabaya.

Akiendelea,amesisitiza kuwa, “Wamejaribu kutuharibu, lakini hatukubaliani nao Mke na mke wakioana hawawezi kuzaa, na mume na mme wakioana hawawezi kuzaa.

Wasira amekumbusha kuwa CCM itaendelea kuongoza kwa imani ya Watanzania na kwamba wataendelea kutunza amani na kuimarisha maendeleo ya nchi. Alisema, “Msiwache watoto wetu wakaharibike, mzingatie malezi na mhakikishe nchi yetu inaendelea kuwa nchi bora.”

Akizungumzia mchango wa Rais Samia Suluhu Hassan katika maendeleo ya Tanzania, Wasira amesema Rais Samia amefanya kazi nzuri katika kipindi cha uongozi wake, na amevunja rekodi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Kwa upande mwingine, Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Mary Chatanda, ameipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa utekelezaji mzuri wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020-2024.

Kwaupande wake makamu mwenyekiti UWT Zainab Shomari amesema kuwa UWT ni jeshi kubwa la kweli, likiwa na idadi kubwa ya wanawake kutoka sehemu mbalimbali  nchini.


Post a Comment

0 Comments