SERIKALI YAIPONGEZA NMB KWA KAMPENI YA KIJIJI DAY

 


📌BAHATI MSANJILA

Serikali wilaya ya Kilosa imesema benki ya NMB imekuwa ikifanya vizuri na ni taasisi ya kuigwa katika kujenga mahusiano yake na jamii zinazowazunguka na serikali kwa ujumla. 

Mkuu wa wilaya ya Kilosa Shaka Hamdu Shaka amebainisha hayo Kijiji cha Msowero wilayani Kilosa wakati anafungua NMB Kijiji Day, ambapo katika siku hiyo benki ya NMB inafanya michezo mbalimbali na wanakijiji husika, kutoa elimu ya fedha kwa wananchi na vikundi vya wajasiriamali katika eneo hilo lengo la Kijiji day likiwa kila mtanzania popote pale alipo awe na uelewa wa kutosha juu ya masuala ya fedha na kunufaika na fursa zinazotolewa na taasisi za kifedha hapa nchini 

Mkuu wa Wilaya Shaka amesema ni ukweli usiopingika kuwa benki ya NMB imekuwa ikigusa Maisha ya watanzania hadi yule wa chini kabisa kutokana na mifumo yake ya urejeshaji kwa jamii ilivyojiwekea, ambapo katika NMB Kijiji Day kijijini MSOWERO licha ya kutoa elimu ya fedha na kufungulia wananchi akaunti, pia waliambatana na kampuni za zana za kilimo na nishati safi ya kupikia ambao nao pia walitoa elimu kwa wanavijiji hao. 

Kwa upande wao benki ya NMB kupitia meneje wa NMB kanda ya Kati Janeth Shango Amesema NMB Kijiji Day ambayo lengo lake kuu ni kuhakikisha kila mtanzania popote pale alipo anapata elimu ya fedha, wamekuwa wakitumia siku hiyo pia kutoa elimu ya masuala ya utawala bora, bima , kilimo biashara pamoja na mikopo kwa vikundi mbalimbali vya wajasiriamali vilivyopo vijijini. 

Benki ya NMB imeanzisha kampeni maalumu inayoitwa NMB KIJIJI DAY lengo likiwa kuhakikisha hakuna mtanzania anaeachwa nyumba katika kupata elimu ya fedha, na katika kampeni hiyo pia benki ya NMB inahakikisha kila Kijiji hapa nchini kinakuwa na MAWAKALA WA BENKI YAKE wasiopungua wawili ili dhana nzima ya huduma za kifedha jumuishi liweze kufanikiwa kwa vitendo.







 

Post a Comment

0 Comments