📌BAHATI MSANJILA
Maelfu ya vijana wamejitokeza jijini Dodoma kushiriki CCM @48 Marathon, ikiwa ni sehemu muhimu ya maadhimisho ya miaka 48 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Mbio hizi zinahitimishwa katika Viwanja vya
Jakaya Kikwete Convention Centre, huku Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, John
Mongella, akiongoza shughuli za CCM Marathon, ikiwa ni muendelezo wa maandalizi
kuelekea maadhimisho ya miaka 48 ya chama hicho.
Viongozi wengine walioshiriki mbio hizo ni
Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Mohammed Kawaida, Katibu Mkuu wa UVCCM, Jokate
Mwegelo, na Katibu wa NEC Organization, Issa Gavu.
Mwenyekiti wa Chama Taifa na Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika
hafla ya kutimiza miaka 48 ya CCM, itakayofanyika tarehe 5 Februari 2025.
0 Comments