KAWAIDA AKAGUA MAANDALIZI YA CCM @48 MARATHON, AHAMASISHA VIJANA KUSHIRIKI

 


📌BAHATI MSANJILA

Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Mohammed Kawaida, amekagua maandalizi ya CCM @48 Marathon yanayofanyika Dodoma, ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Miaka 48 ya CCM. Kawaida amewataka vijana kujitokeza kwa wingi kushiriki mbio hizo, akisisitiza kuwa maandalizi yamekamilika na wataweza kupokea zaidi ya vijana 15,000 watakaoshiriki.

Amesema kuwa mbali na mbio, kutakuwa na shughuli mbalimbali za burudani, ikiwa ni pamoja na furaha, michezo, na nyimbo, zote zikienda sambamba na maandalizi kuelekea tarehe 5 Februari 2025, ambapo CCM itaadhimisha miaka 48 tangu kuanzishwa kwake.

Mgeni rasmi katika mbio hizo anatarajiwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM, na mgombea mwenza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Emmanuel Nchimbi.

Mwenyekiti wa Chama Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika hafla ya kutimiza miaka 48 ya CCM, itakayofanyika tarehe 5 Februari 2025.

 

 


Post a Comment

0 Comments