VITUO VYA ELEKTRONIKI KUONDOA USUMBUFU KWA RAIA WA TANZANIA KATIKA UPATIKANAJI VIBALI SHUGHULI ZA KIJAMII ZAMBIA

 








📌BAHATI MSANJILA.


SERIKALI imeanzisha mifumo ya ki-elektroniki katika vituo vya Mikoa na Wilaya ili kurahisisha upatikanaji wa hati za safari, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuondoa usumbufu kwa raia wa Tanzania wanapohitaji vibali kwa ajili ya kushiriki shughuli za kijamii nchini za jirani.

 

hayo yameelezwa Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Daniel Sillo alipokuwa akijibu swali la Mhe. Josephat Sinkamba Kandege, Mbunge wa Kalambo aliyeuliza Je, lini Serikali itaondoa usumbufu wa kupata vibali na gharama pale raia wa Tanzania wanapolazimika kushiriki shughuli za kijamii nchini Zambia.

 

Akijibu,  swali hilo Sillo ameeleza kuwa, Serikali imetekeleza mifumo ya ki-elektroniki katika ngazi za Mikoa na Wilaya ili kurahisisha upatikanaji wa hati za safari, pasipoti, na hati za dharura Lengo ni kuwaondolea wananchi usumbufu wanapohitaji vibali vya kushiriki shughuli za kijamii katika nchi jirani .

 

Vilevile, Mhe. Sillo amesema kuwa raia wa Tanzania wanaoishi katika maeneo ya kilometa 10 kutoka mpaka wa Tanzania  wanapewa vibali maalum kwa ajili ya kushiriki shughuli za kijamii, kama misiba na matukio ya dharura, bila gharama kubwa.

 

Ameongeza kwa kusema kuwa Kwa raia wanaoenda nchi jirani kwa ajili ya shughuli za kiuchumi, wanapaswa kufuata Sheria na Taratibu za nchi hiyo, pamoja na kulipia vibali vinavyohusiana na shughuli zao.

 

Hatua hii ya mifumo ya ki-elektroniki ni sehemu ya juhudi za Serikali kuboresha huduma kwa wananchi na kuondoa changamoto za urasimu, huku pia ikifungua fursa za kiuchumi kwa raia wa Tanzania wanaoshiriki shughuli mbalimbali katika nchi jirani.





 

 


Post a Comment

0 Comments