📌BAHATI MSANJILA
Serikali imetoa ufafanuzi
kuhusu madai ya maiti kuzuiliwa hospitalini kutokana na deni la matibabu,
ikisisitiza kuwa suala hilo si jukumu la madaktari bali ni la uongozi wa
hospitali husika.
Akijibu swali la Mbunge wa Segerea, Mhe. Bonna
Ladislaus Kamoli, Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel amesema kuwa katika
ufuatiliaji uliofanywa ili kuchukua hatua za kinidhamu, imebainika kuwa mara
nyingi ndugu wa marehemu hukataa kufuata utaratibu uliowekwa, jambo
linalochangia ucheleweshaji wa kutoa miili.
Aidha ameeleza kuwa baadhi ya ndugu huchagua
kulalamika kwa vyombo vya habari na viongozi badala ya kushughulikia taratibu
zinazopaswa kufuatwa.
Ameongeza kuwa Serikali imeeleza kuwa tayari
imetoa waraka namba moja wa mwaka 2021 unaoelekeza kutoruhusu maiti kuzuiliwa
hospitalini kwa sababu ya madeni ya matibabu.
Dkt. Mollel amesema Waraka huo umeweka utaratibu
wa kulipa gharama hizo bila kuathiri utoaji wa huduma kwa wafiwa.
Amesisitiza kuwa Serikali inasimamia utekelezaji
wa miongozo hiyo ili kuhakikisha haki za wananchi zinalindwa, huku akihimiza
ndugu wa marehemu kushirikiana na uongozi wa hospitali kufuata taratibu
zinazostahili.
0 Comments