BITEKO AZINDUA MIKOPO YA NMB KWA WASAMBAZAJI WA NISHATI SAFI,BILI0NI 100 ZATENGWA.

 


📌BAHATI MSANJILA 


NAIBU Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano waTanzania Doto Biteko ambae pia ni Waziri wa Nishati amezindua mikopo kwa wasambazaji nishati safi nchini inayotolewa na benki ya NMB, huku akibainisha wazi kuwa kukosekana kwa mitaji kwa wasambazaji wa nishati hiyo ni moja ya kikwazo cha kampeni hiyo iliyoasisisiwa na rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan. 

Benki ya NMB imetenga jumla ya shillingi billion mia moja kwaajili ya mikopo kwa wasambazaji wa nishati safi na salama, mikopo inayotolewa kwa riba ya asilimia moja kwa mwezi huku kiwango cha juu cha mkopo huo kwa mfanyabiashara mmoja kikiwa shillingi billion moja, lengo likiwa nishati hiyo iweze kufika kila kona ya tanzania.. 

Naibu waziri mkuu ambae pia ni waziri wa nishati, amesema tafiti zilizofanyika toka kuanza kwa kampeni ya matumizi ya nishati safi na salama hapa nchini wamebaini kuwa moja ya sababu inayokwamisha ufanisi wa kampeni hiyo ni kutokuwepo kwa vituo vya kuuzia nishati safi ambavyo vipo karibu na wananchi hasa maeneo ya vijijini, hivyo kitendo cha benki ya NMB kuanza kutoa mikopo hiyo kwa wasambazaji wa nishati safi, inakwenda kutatua tatizo hilo . 

Kwa upande wao benki ya NMB kupitia afisa mtendaji mkuu wake Ruth Zaipuna amesema benki imetenga shilling billion mia moja  za mikopo ili upatikanaji wa nishati  safi kwa watanzania uwe wa rahisi na kwamba mkopo huo huo ambao kiwango cha juu cha mkopaji ni billion moja utalipwa ndani ya miaka miwili, riba kwa mwezi ikiwa ni asilimia moja. 

Katika kuhakikisha watanzania wengi Zaidi wanafikiwa na nishati safi na salama, benki ya NMB kwa kushirikiana na Tais Gas wataendesha kampeni ya kuelimisha watanzania kupitia NMB KIJIJI DAY, ambapo kwa mwaka 2025 wanatarajia kuvifikia jumla ya vijiji 2000.

 






Post a Comment

0 Comments