CHUO MAHIRI CHA TEHAMA KUJENGWA NALA DODOMA-WAZIRI SILAA

 ðŸ“ŒBAHATI MSANJILA

SERIKALI kupitia Wizara ya Habari  Mawasiliano  na Teknolojia ya Habari  imesema inatarajia kujenga  chuo  Mahiri cha TEHAMA (Digital Technology Institute) Nala Dodoma, lengo likiwa ni kusaidia kuchochea  ukuaji wa sekta hiyo nchini.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Jerry Silaa, leo Disemba 5,2024 jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Silaa amesema ujenzi wa chuo hicho ni wanatekeleza agizo la Rais Dkt.  Samia Suluhu Hassan,ambapo alielekeza  chuo hicho kijengwe ili kusaidia kuchochea Sekta ya TEHAMA huku akisema, kuna vijana wengi ambao wana ubunifu na kuna vyuo vikuu vingi ambavyo  vinafanya bunifu, hivyo ujio wa chuo hicho itakuwa ni kituo cha  kuboresha na kuwasaidia wabunifu hao.

Kazi ya chuo hicho kama nilivyosema itakuwa ni Center ya kuwasaidia vijana wengi, kampuni za vijana ambao wanakuwa na bunifu ambazo zinatoa suluhu za kitehama  kwaajili ya kutatua matatizo mbalimbali ya kijamii  kwenye sekta zote kama vile , kilimo  sekta za afya chuo hicho kinaenda kuziba hilo pengo baina ya  bunifu za vijana wetu  ambao wanajitengenezea ajira zao wenyewe

Vilevile pia chuo hicho kitaweza kuwasaidia wabunifu kupata ufahamu wa sekta mbalimbali jinsi ya kufungua kampuni zao na jinsi kuweza kuwa na bunifu na bunifu zipate maeneo ya kufanyia majaribio, na chuo hiki  moja ya kazi yake  itakuwa ni kukusanya bidhaa za kitehama ambazo zinaweza kuuzika nje ya nchi

 Silaa

Amesema mradi wa chuo hicho cha Tehama una pande mbili, chini ya mradi mkubwa wa  Digital  Tanzania  Project ambao unafadhiliwa na  Benki ya Dunia na umesaidia katika masuala ya uaandaji wa mtaala na  majadiliano mbalimbali wa chuo hicho.

Hata hivyo amesema mpaka sasa Wizara ya Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari imepata eneo Nala Dodoma la ekari 400 na maandalizi ya mradi yanaendelea ambapo tayari upembuzi yanikifu umefanyika, na mradi upo katika hatua za mwisho za majadilino  ili ujenzi uanze na ndani ya miaka miwili wanatarajia kuwa chuo hicho kitakuwa kimeshakamilika.

Post a Comment

0 Comments