📌 BAHATI MSANJILA
Katibu Mkuu wa Umoja wa
Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), Cde. Jokate Mwegelo, ameonyesha tena nia
ya kuimarisha ustawi wa vijana nchini kwa kuchangia Shilingi milioni tatu kwa
bodaboda wa kituo cha Sabasaba A, maarufu kama “Vijana na Samia,” mkoani Dodoma.
Mchango
huo unalenga kuwawezesha vijana hao kuboresha huduma zao na kuimarisha mfuko wa
maendeleo wa kituo hicho. Uzinduzi wa shina la Wakereketwa la UVCCM la “Vijana
na Samia” ulifanyika sambamba na kukabidhiwa kibanda maalum kwa ajili ya
kupumzikia, kilichojengwa kwa msaada wa Mbunge wa Dodoma Mjini, Ndg. Anthony
Mavunde.
Akizungumza
katika tukio hilo, Cde. Jokate aliwataka vijana hao kuendelea kuwa na imani na
serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, akibainisha juhudi kubwa
zinazofanyika kuhakikisha vijana wanapewa nafasi na msaada wa kushiriki
kikamilifu katika uzalishaji na maendeleo ya kiuchumi.
Serikali ya Rais Samia imejikita katika kuwawezesha vijana, na nyinyi ni sehemu muhimu ya mabadiliko hayo. Endeleeni kuwa mstari wa mbele kuunga mkono juhudi hizi,
Kabla
ya tukio hilo, Cde. Jokate aliongozana na vijana zaidi ya 500 waliokuwa
wakihamasisha maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCM unaotarajiwa kufanyika
Januari 18 hadi 19, 2025, katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete. Vijana
hao walionyesha mshikamano na hamasa kubwa, wakiendelea kuipa nguvu kauli mbiu
ya chama “Kijana na Kijani.”
Mbunge
wa Dodoma Mjini, Ndg. Anthony Mavunde, alisisitiza umuhimu wa kuboresha
mazingira ya kazi kwa vijana na kuahidi kuendelea kushirikiana nao kwa karibu.
Kibanda cha kupumzikia kilichozinduliwa sasa kitasaidia bodaboda kujikinga
dhidi ya jua na mvua wakati wa shughuli zao za kila siku.
Uzinduzi
wa shina hilo ni moja ya hatua muhimu za UVCCM katika kuhakikisha vijana
wanashiriki kikamilifu katika maendeleo ya jamii na kuimarisha mshikamano ndani
ya chama.
0 Comments