CHUO KIKUU MZUMBE CHASAINI HATI YA MAKUBALIANO NA USHIRIKIANO NA CHUO KIKUU CHA BONN

 




📌Na Mwandishi wetu, Morogoro.

MAKAMU  Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe Prof. William Mwegoha amesema, Mzumbe iko tayari kushirikiana na wadau wengine wa ndani na nje ya nchi katika kubadilishana uzoefu katika maeneo ya taaluma na tafiti.
Prof. Mwegoha amesema hayo mwishoni mwa wiki wakati wa hafla ya kusaini hati ya makubaliano kati ya Chuo Kikuu Mzumbe na Chuo Kikuu cha Bonn yanalolenga kuimarisha uhusiano wa kitaaluma na kuboresha ubora wa elimu, utafiti na ubunifu baina ya vyuo hivyo.

Awali,Prof. Detlef Mueller-Mahn kutoka Chuo Kikuu cha Bonn amesema ni fursa kwao kuimarisha ushirikiano utakaoleta tija baina vyuo hivyo kwa kuinua viwango vya elimu ya juu na utafiti katika nyanja mbalimbali huku ukihimiza uvumbuzi na ubunifu.

Makubaliano hayo ya ushirikiano yanaelekezaushiriki wa Chuo Kikuu Mzumbe katika miradi ya utafiti na kuboresha mitaala ilikukidhi mahitaji ya soko ya ajira kimataifa. Pia, ushirikiano huo utaleta fursaza semina, warsha na kongamano za kitaaluma zinazolenga kujadili changamoto nambinu bora za kuboresha elimu na utafiti.

Hati ya makubaliano baina ya Chuo Kikuu Mzumbe na Chuo cha Bonn ni ya miaka mitano kufuatia kukamilika kwa awamu ya kwanza ambapo wanataaluma wamenufaika na fursa za masomo na tafiti katika nyanja za taaluma na tafiti.

 







Post a Comment

0 Comments