JKT YATOA WITO VIJANA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA

 ðŸ“ŒRUCIANA NYONI

MKUU wa Jeshi la kujenga taifa (JKT) Meja Jenerali Rajabu Mabele, anawataarifu vijana wote wa Tanzania Bara na visiwani nafasi ya kujiunga na mafunzo ya jeshi la kujenga Taifa kwa mwaka 2023.

Taarifa hii imetolewa Leo Agosti, 25 2023 na Mkuu wa Tawi la Utawala Jeshi la Kujenga Taifa JKT Brigedia Jenerali Hassan Mabena,akizungumza na Waandishi wa Habari  leo Agosti 25,2023 Makao Makuu ya JKT Chamwino Mkoani Dodoma kwa niaba ya MKUU wa JKT Meja Jenerali  Rajabu Mabele 

Usahili wa vijana hao wa kujiunga na mafunzo ya Jeshi la kujenga Taifa kwa kujitolea  utaanza tarehe 28 Agosti, 2023 kwa mikoa yote ya Tanzania bara na visiwani vijana watakaochaguliwa wanatakiwa kuripoti makambini kuanziaa tarehe 26 Septemba hadi tarehe 29 Septemba  2023.

Vijana watakao ripoti makambini wanatakiwa  kuripoti na vifaa ambavyo ni bukta ya rangi ' Dark blue' yenye mpira  kiunoni (lastic) iwe na mfuko mmoja nyuma urefu unaoishia magotini isiyo na zipu  kwa vijana wa kike iwe na mpira kiunoni na kwenye pindo za miguu, Raba za michezo rangi ya kijani au blue , shuka mbili za kulalia rangi ya blue bahari , soksi ndefu nyeusi nguo za kuzuia baridi kwa wale watakaochaguliwa kwenye mikoa ya baridi

Mabena 

Utaratibu wa kuomba na kujiunga na mafunzo hayo unaratibiwa na Ofisi za wakuu wa Mikoa na wilaya ambako  muombaji anaishi.

Sifa za muombaji lazima awe raia wa Tanzania  wenye elimu ya darasa la Saba awe na umri kuanzia miaka 16 hadi 18  waliomaliza elimu ya msingi kuanzia mwaka  2020, 2021,2022 awe na cheti halisi cha kumaliza elimu ya msingi na kwa kwa wale wenye elimu ya kidato cha nne umri usizidi  miaka 20 awe amemaliza elimu ya sekondari kuanzia 2020, 2021 na 2022 awe na cheti halisi cha kumaliza  elimu ya sekondari ( leaving certificate) na cheti halisi cha matokeo  ( academic certificate) na awe na ufaufu wa daraja la kwanza hadi  daraja la nne, kijana mwenye daraja la nne awe na ufaufu kuanziaa  26 hadi 32 na kidato cha sita umri usizidi miaka 25  awe amemaliza elimu ya sekondari kuanziaa 2020, 2021, na 2022.

Pia kwa  elimu ya stashahada umri usizidi miaka 25  awe na  cheti cha sekondari na chuo, awe na akili timamu asiwe na michoro yeyote ( tattoo), awe na tabia  na nidhamu nzuri hajawahi kupata hatia yeyote mahakamani wala kufungwa,  asiwe ametumika jeshi la polisi, magereza, chuo Cha mafunzo au kikosi maalumu cha kuzuia magendo au kuajiriwa katika idara yeyote selikarini, asiwe amejihusisha na madawa ya kulevya bangi na yanayofanana na hayo

Mabena

Kijana atakayepatikana na nyaraka za kughushi atachukuliwa hatua kali za kisheria kulingana na taratibu zilizopo. 

Aidha jeshi la kujenga Taifa linapenda kuwataarifu vijana watakaopata fursa  hiyo kuwa halitoi ajira pia halihusiki  kuwatafutia ajira katika asasi, vyombo vya ulinzi na usalama .

Mkuu wa (JKT ) Meja Jenerali  Rajabu Mabele anawakaribisha vijana wote watakaopata fursa ya kujiunga na vijana wenzao ili kujenga  uzalendo, Umoja wa kitaifa, Ukakamavu,  kufundishwa stadi za kazi, stadi za maisha na utayari wa kulijenga na kulitumikia Taifa lao na mashirika mbalimbali ya kiserikali na yasio ya kiserikali.

 

Post a Comment

0 Comments