THRDC YAWAFUA MAHAKIMU NA MAJAJI KUHUSU WAJIBU MAHAKAMA KATIKA KUTUNZA NA KULINDA UHURU

 ðŸ“ŒJASMINE SHAMWEPU

MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umetoa mafunzo ya siku mbili kwa Mahakimu na Majaji kuhusu wajibu wa Mahakama katika kutunza na kulinda uhuru wa kujieleza pamoja na haki za binadamu nchini.

Mratibu wa Mtadao wa THRDC, Onesmo Olengurumwa akizungumza na waandishi wa habari leo jijini hapa, wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo kwa Mahakimu na Majaji nchini alisema lengo ni kukumbushana wajibu katika kutekeleza majukumu ya kila siku.

Lengo la mafunzo haya ni kukumbushana masuala mbalimbali katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku, kumekuwepo na mabadiliko mengi ya kisheria na masuala mbalimbali yanayohusu haki za binadamu hivyo wao kama watu ambao wanatoa haki kila siku katika Mahakama, wanapaswa kuyafahamu ili kulinda haki za binadamu na uhuru wa kujieleza

Olengurumwa

Amesema pia mafunzo mengine ambayo yatatolewa ni masuala ya maadili kwa Mahakimu na Majaji katika utekelezaji wa majukumu ya utoaji wa haki katika maeneo yao.

Suala la maadili ni jambo la muhimu sana katika mahakama zetu nchini hivyo mafunzo haya pia yatasaidia kuwakumbusha Mahakimu na Majaji wajibu wao wa kutenda haki kwa kuzingatia maadili ya kazi zao

Olengurumwa

Amesema utoaji wa mafunzo hayo ni sehemu ya Mtandao huo kuunga juhudi za serikali katika kuboresha miundombinu ya utoaji haki nchini.

Tusiwe watu wa kulalamika tunapaswa kushiriki kuboresha Mahakama zetu kufanya kwa pamoja kama taifa huduma ya Mahakama ni huduma ya haki jukumu letu kusaidia kuboresha sekta hii ili kupunguza malalamiko yaliyopo kwa wananchi katika masuala ya haki jinai

Olengurumwa

Naibu katibu mkuu wa Chama cha Mahakimu na Majaji Tanzania (JMAT) Mary Kallomo, amesema mafunzo hayo yatawasaidia kuboresha utendaji wao wa kila siku katika kulinda haki za binadamu na uhuru wa kujieleza.

Tunahitaji kukumbushana masuala mbalimbali katika utekelezaji wa majukumu yetu na suala la maadili ni jambo la muhimu sana kwakuwa sisi ndiyo tunatoa haki katika Mahakama zetu

Hata hivyo, amesema ipo haja kwa wadau wa masuala ya haki jinai nchini kutoa mafunzo kwa kundi hilo kuhusu masuala ya kimtandao.

Teknolojia hivi sasa imekuwa sana hivyo kutokana na hali hiyo ipo haja Mahakimu na Majaji kupatiwa mafunzo ya masuala ya kimtandao ili wanapotoa huduma zao wasivunje haki za binadamu pamoja na uhuru wa kujieleza

Kallomo

 

Post a Comment

0 Comments