RC MTAKA AWAONYA WAKANDARASI MIRADI YA MAJI

 


📌RHODA SIMBA

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Antony Mtaka amewataka wakandarasi wanaotekeleza miradi ya maji zitokanazo na fedha za UVIKO 19 kukamilisha kwa wakati na kwa ufanisi.

Mtaka ameyasema hayo jijini hapa wakati  wa hafla fupi ya kusaini mikataba ya ujenzi wa miradi ya maji kati ya makandarasi na  mamlaka ya maji  vijijini (RUWASA)Mkoa wa Dodoma.

Amesema kwa mkandarasi atakaye tekeleza miradi hiyo chini ya kiwango na nje ya mkataba Mkoa hautampatia kazi nyingine tena.

Niseme tu kwamba kwa mkandarasi  atakayeshindwa kutekeleza miradi yake kwa muda na kwa ufanisi hatutampatia kazi tena (tutamblacklist)  kwani lengo ni kwamba kwenda na kasi ili kazi zikamilike mapema

RC Mtaka

Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Fatuma  Mganga amesisitiza miradi hiyo ifanyikekwa ufanisi na kwa kiwango cha thamani ya fedha iliyotolewa ili kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan katika kuwaletea wananchi wake maendeleo.

Awali akisoma taarifa fupi ya utekelezaji wa miradi hiyo kwa Mkuu wa Mkoa Meneja wa Ruwasa Mkoa  Dr Godfrey Mbabaye amesema mikataba inayosainiwa imegawanyika katika makundi mawili.

Amesema mkoa wa Dodoma ulitengewa kiasi cha shilingi billion 3.9 kutekeleza miradi 8 katika Wilaya za Kongwa,Chamwino,Kondoa Chemba na Mpwapwa.

Mikataba inayotarajiwa kusainiwa leo ni mikataba miwili ya Wilaya za Chamwino,Chemba  na Kondoa yenye jumla ya miradi mitano ambapo thamani ya mikataba hiyo ni shilingi bilioni 1.9

Mbabaye.

Amesema mkataba mmoja wenye miradi mitatu ya Wilaya ya Kongwa,na Mpwapwa wenye thamani ya shilingi billion 1.6 umepelekwa kwa mwanasheria Mkuu wa Serikali kwaajili ya kufanyia upembuzi na unategemewa kusainiwa kabla ya January 16 2022.

“Miradi inayotumia fedha za ndani inayotegemewa kusainiwa leo ni miwili ambayo itatekelezwa katika wilaya za Chamwino na Kondoa na miradi hiyo inajumla  ya shilingi bilioni 1.7” amesema Mbabaye

Post a Comment

0 Comments