Mkuu huyo wa Wilaya, ameyasema
hayo jijini Dodoma, wakati alipokuwa akizindua maduka ya GSM ya nguo na samani
za maofisi na majumbani.
Maganga, amesema kuwa serikali
hivi sasa imeondoa urasimu pamoja na milolongo mirefu kwa wawekezaji ili
kuwezesha upatikanaji wa vibali kuchukua muda mfupi kama ambavyo Rais aliagiza
wakati akizindua Bunge la 12.
Amesema, jiji la Dodoma bado
linayo ardhi ya kutosha kwa ajili ya kuwekeza huduma mbalimbali kama vile sekta
ya afya, elimu, miundombinu pamoja na viwanda.
Amesema Hali hiyo itasaidia
kuongeza wawekezaji wengi kutokana na mazingira rafiki yaliyopo ikiwemo agiza
la Rais kutaka vibali vya wawekezaji kutolewa ndani ya siku 14.
0 Comments