POLISI DODOMA YATOA ONYO UTAPELI MKUTANO MKUU CCM




JESHI la Polisi Mkoa wa Dodoma kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama limejipanga kudhibiti vitendo vya utapeli kwa washiriki wa uchaguzi

Akizungumza na waandishi wa habari  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma , Gilles Muroto amesema wamejipanga kudhibiti vitendo hivyo ili mkutano huo ufanyike kwa usalama na amani

Jeshi limejipanga kuhakikisha yeyote atakayejaribu kufanya utapeli wa kujifanya yupo karibu na viongozi wakuu wa kitaifa hawataondoka Dodoma, wajipange kubakia ili kushughulikiwa kwa mujibu wa sheria
RPC Muroto.


RPC Muroto amesisitiza kuwa hatotaka kuona vitendo vya utapeli katika mkutano huo unaohudhuriwa na viongozi wakuu wa kitaifa, viongozi wa Serikali wastaafu, viongozi wa vyama rafiki wa CCM kutoka mataifa mbalimbali duniani na kutoka katika mikoa mbalimbali.

Muroto amesema mkutano huo unaotarajiwa kuwa na wajumbe zaidi ya 3,000 hatopenda kuona watu wanatenda vitendo vya kitapeli  kwa kutumia ukaribu au majina ya viongozi.

Amesema uzoefu unaonesha katika mikutano kama hiyo pia wamekuwa wakihudhuria  watu wenye nia ovu ambao wanatumia fursa hiyo kutekeleza azma yao ya kitapeli.

Muroto amesema jeshi hilo limejiandaa kikamilifu kukabiliana na vitendo hivyo vya kitapeli kabla havijatokea .



Post a Comment

0 Comments